Klabu ya PSG kutoka Ufaransa imepata ushindi dhidi ya Chelsea mechi ya mkondo wa kwanza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Benfica nao wakilaza Zenit St-Petersburg.
Paris St-Germain walichukua uongozi kupitia mshambuliaji matata wa Sweden Zlatan Ibrahimovic dakika ya 39.
Chelsea walisawazisha katika dakika ya 45 kupitia kwa Mikel Obi lakini Edison Cavan akaitumia dakika ya 78 kuwaumiza Chelsea.
Bao hilo la Mikel ndilo lake la sita kufungia Chelsea katika karibu miaka 10 aliyokaa katika klabu hiyo ya Uingereza.
... Read more »