Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
10:58 AM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 3
Guests: 3
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 17

 

“Ukweli katika nchi hii soka lipo lakini ni hali ya kusikitisha mno kuona hakuna wafadhili wanaojali na kuthamini vipaji vya wanasoka hasa vijana, inaniuma sana hali hii hasa ninapoona vijana tunatumia nguvu za ziada kufanya mambo muhimu kama kujituma na kucheza soka vizuri na hakuna anaetuona wala kutujali, sijui hali hii itatuondoka lini”

... Read more »

Views: 247 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

Mwanamasumbwi Manny Pacquiao amelazimika kuomba radhi kutokana na upinzani mkubwa alioupata kutoka kwa wale wanaounga mkono uhusiano ya jinsia moja.

Sakata hili limeanza pale ambapo Pacquaio ambaye pia ni mbunge huko kwao ufilipino aliposema kupitia televisheni kuwa matendo ya jinsia moja ni mabaya kuliko ya wanyama.

Mwanandondi huyo alise ... Read more »

Views: 195 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

 

Mashabiki wa Manchester United wana mpango wa kuipinga Bei ya pauni 71 wanayotakiwa kulipia ili kuona mechi yao ya Europa Ligi dhidi ya Midtjylland hapo kesho.

Mechi kama hiyo hiyo mashabiki wa Southampton walitozwa pauni 22 sasa Mashabiki wa Manchester United wanalalamika wanasema kwani waliopanga viingilio wanadhani mashabiki wa manchester ni matajiri mara tatu zaidi ya mashabiki wa Southampton? ... Read more »

Views: 142 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

 

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ameondoka kwa hasira katika katika chumba cha mahojiano baada ya kuulizwa juu ya rekodi ya ufungaji magoli katika mechi za ugenini msimu huu.

 

Ronaldo mwenye miaka 31, amefunga magoli 32 msimu huu lakini hajafunga nje tangu mwezi Novemba."Nani mwingine amefunga magoli mengi ugenini kuliko mimi tangu nimekuja Hispania? Aliuliza Ronaldo mfungaji namba moja wa Championzi Ligi"Taja mchezaji mmoja ambaye amefunga kuliko mimi. Hakuna jibu? Sawa. Asante" Akaondoka.

 

Ronaldo alikuwa akiongea na wanahabari kab ... Read more »

Views: 204 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

 

Katika Mechi ya Fainali ya mashindano ya voliboli ya wanawake afrika yaliyomalizika mjini Yaounde hapo jana, Cameroon imeishinda Misri kwa seti 3-2.

Kwa ushindi huo Cameroon italiwakilisha bara Afrika katika michezo ya Olimpiki mwezi Agosti mjini Rio Brazil.

Katika mechi ya kuwania mshindi wa tatu Kenya imewashinda Algeria seti 3-0 na kuzoa nishani ya shaba. ... Read more »

Views: 178 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

Nchini Tanzania Gumzo miongoni mwa wapenzi wa Soka ni kuhusiana na Mechi kubwa ya watani wa Jadi vilabu vikongwe vya Yanga na Simba itakayofanyika mwishoni mwa juma lakini kubwa zaidi sasa linalojadiliwa ni baada ya shirikisho la Soka nchini humo kutangaza kuwa mwamuzi wa mchezo huo ni mwanamama Jonesia Rukiyaa.

Mitandao inasema mwanadada huyo ni mmoja wa marefa ambao wanasimamia sheria za uwanjani kwa hak ... Read more »

Views: 217 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

Mkuu wa Riadha nchini Kenya amesema anataka kuachia ngazi kwa muda baada ya tuhuma kuwa aliwataka wanariadha kumhonga ili kupunguziwa kifungo kutokana na utumiaji wa dawa za kusisimua misuli.

Isaac Mwangi anakanusha tuhuma hizo na anataka kuiachia nafasi yake kwa siku 21 wakati Shirikisho la Riadha Duniani likifanya uchunguzi. "Tuhuma hizi zimenisababishia usumbufu mkubwa wa mawazo" Mwangi alisema"Ningependa jina langu lisafishwe"

Wanariadha wawili waliosimamishwa walidai Mwangi aliwataka kutoa fedha ili wap ... Read more »

Views: 188 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

 

Klabu ya PSG kutoka Ufaransa imepata ushindi dhidi ya Chelsea mechi ya mkondo wa kwanza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Benfica nao wakilaza Zenit St-Petersburg.

Paris St-Germain walichukua uongozi kupitia mshambuliaji matata wa Sweden Zlatan Ibrahimovic dakika ya 39.

Chelsea walisawazisha katika dakika ya 45 kupitia kwa Mikel Obi lakini Edison Cavan akaitumia dakika ya 78 kuwaumiza Chelsea.

Bao hilo la Mikel ndilo lake la sita kufungia Chelsea katika karibu miaka 10 aliyokaa katika klabu hiyo ya Uingereza.

... Read more »

Views: 186 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)

Mshikemshike wa ligi kuu soka visiwani Zanzibar kanda ya Unguja, leo ukiendelea katika kiwanja cha Amani kwa mzunguko wake wa pili ambao ni wa lala salama, Jang’ombe boys watamenyana na Timu ya Kimbunga leo jioni ndani ya dimba la Amani.

Katika mchezo wa awali walipokutana Jang’ombe walikubali kufungwa na Kimbunga mabao 2-1, mchezo ambao Jang’ombe walikuwa ugenini.

... Read more »

Views: 173 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.17.2016 | Comments (0)


Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz