Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
11:50 PM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 17 » CHELSEA WALAZWA NA PSG LIGI YA MABINGWA.
8:17 AM
CHELSEA WALAZWA NA PSG LIGI YA MABINGWA.

 

Klabu ya PSG kutoka Ufaransa imepata ushindi dhidi ya Chelsea mechi ya mkondo wa kwanza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Benfica nao wakilaza Zenit St-Petersburg.

Paris St-Germain walichukua uongozi kupitia mshambuliaji matata wa Sweden Zlatan Ibrahimovic dakika ya 39.

Chelsea walisawazisha katika dakika ya 45 kupitia kwa Mikel Obi lakini Edison Cavan akaitumia dakika ya 78 kuwaumiza Chelsea.

Bao hilo la Mikel ndilo lake la sita kufungia Chelsea katika karibu miaka 10 aliyokaa katika klabu hiyo ya Uingereza.

Bao pekee la Benfica, waliokuwa nyumbani, lilifungwa na Jonas muda wa ziada kutokana na mkwaju wa adhabu uliopigwa na Nicolas Gaitan.

Hilo ndilo bao lake la 25 msimu huu na la 45 kufungia Benfica katika mechi 56 tangu alipojiunga nao akitokea Valencia mwaka 2014.

Zenit walisalia wachezaji kumi uwanjani baada ya Domenico Criscito kupewa kadi ya pili ya njano dakika ya 90.

Katika ligi Championship nchini Uingereza, Blackburn Rovers walishinda 3-0 dhidi ya Fulham nao Hull City wakatoka sare 0-0 na Brighton & Hove Albion.

Views: 187 | Added by: salminjsalmin | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar

Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz