Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
6:08 PM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 18

Katika Afrika ya Kati kulikuwa na Mechi ya Ligi ya Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambapo nyasi za Uwanja wa Frederic Kibassa Maliba mjini Lubumbashi zilikuwa zinawakutanisha wafalme wa Ligi ya Mabingwa Afrika TP Mazembe dhidi ya FC Saint Eloi Lupopo lakini hakuna aliyeliona lango la mweziye ijapokuwa Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu alitikisa nyavu kwa Kichwa lakini kumbe alikuwa tayari ameotea.

TP Mazembe sasa wanachangamsha misuli kujiandaa na mechi ya Super Cup ya Afri ... Read more »

Views: 163 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Mshikemshike wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja ikiendelea leo hii kwa kizikutanisha timu ya Jeshi la kujenga uchumi Zanzibar (JKU) na Mafunzo, ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar majira ya saa kumi za jioni.

JKU ambae ni makamo bingwa wa ligi kuu hapa visiwani wataingia uwanjani wakiwa ndio wanaoongoza ligi hiyo wakiwa na alama (31), huku bingwa mtetezi timu ya Mafunzo wataingia uwanjani wakiwa nafasi ya saba (7) na alama zao ni kumi na nane (18).

Katika mzun ... Read more »

Views: 551 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Katika Afrika ya Kati kulikuwa na Mechi ya Ligi ya Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambapo nyasi za Uwanja wa Frederic Kibassa Maliba mjini Lubumbashi zilikuwa zinawakutanisha wafalme wa Ligi ya Mabingwa Afrika TP Mazembe dhidi ya FC Saint Eloi Lupopo lakini hakuna aliyeliona lango la mweziye ijapokuwa ... Read more »

Views: 274 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Katika Uwanja wa El Molinon Lionel Messi amekuwa mchezaji wa kwanza kufikia bao la 300 katika La Liga pale ambapo amepachika mabao mawili dhidi ya Sporting Gijon. Katika mechi hiyo ambayo Sporting wameambulia goli moja, Luis Suarez naye amepiga bao lakini pia akakosa penati.

Messi alifunga la 301 dakika ya 31, wakati lile la Luis Suarez lilikuwa dakika ya 67, huku la wenyeji likifungwa na Castr ... Read more »

Views: 224 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Kilabu ya Miembeni City inayoshiriki ligi soka daraja la pili taifa Unguja imezidi kujikita kileleni mwa kundi A ligi soka daraja la pili taifa Unguja baada yakuifunga timu ya FC Lion jumla ya magol 3-1 ikiwa ni muendelezo wa ligi hiyo mchezo ulichezwa katika kiwanja cha Amani hapo jana mnamo majira ya saa 8 mchana.

City imejikita kileleni mwa kundi A ikiwa na alama 30  baada yakucheza michezo 12 ya mzunguko wa kwanza bila yakupotez ... Read more »

Views: 208 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

FC Midtjylland ya Denmark wameutetea uamuzi wao wa kuwauzia Tiketi mashabiki wa Manchester United kwa pauni 71 wakisema ni suala linaloendeshwa kwa mujibu wa Soko. Bila shaka mahitaji makubwa, yanafanya bei kupanda.

Mashabiki wa United ambao pia leo Timu yao itamkosa Nahodha wao Majeruhi Wayne Rooney ambaye amefunga mabao saba katika mechi zake tisa za mwisho tayari wametengeneza mabango yenye ujumbe wa kulalamika kupinga gharama hiyo wakidai ni kubwa.

Mwezi Ogast ... Read more »

Views: 191 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Christian Ronaldo ni kama amewajibu kwa vitendo wanahabari wale ambao jumanne alikataa kuendelea kuongea nao pale alipoulizwa kuhusu ukame wa magoli ya ugenini. Goli lake la 33 la Musimu limeisaidia Real Madrid kusogelea robo fainali ya Champions Ligi. Kikosi kilichoko chini ya Zinedine Zidane kimeichapa Roma bao mbili kwa moja.

Kabla ya Mechi hiyo Mshambuliaji huyo alikuwa ameondoka kwa ... Read more »

Views: 196 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Kampuni ya utengenezaji vifaa vya michezo ya Nike, imesitisha mkataba na uhusiano na mwanamasumbwi Manny Pacquiao baada ya bondia huyo wa uzito wa juu dunia baada ya kuwafananisha wapenzi wa jinsi moja kama wasio na thamani zaidi ya wanyama.

Bingwa huyo wa masumbwi ulimwenguni mwenye umri wa miaka 37, ambaye anagombea nafasi ya useneta katika bunge nchini mwake Phillipines, ... Read more »

Views: 184 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)

 

Timu ya Jang’ombe boys imeshindwa kutamba baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Kimbunga katika mchezo uliosukumwa jana jioni majira ya saa kumi ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar ambao ni muendelezo mwa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja.

Katika mchezo huo uliojaa mashabiki kiwanjani timu hizo zilionesha kandanda safi kwa kufanya mashambulizi kila mara, na ndipo Waziri Ramadhan alipoweza kuipatia kimbunga bao la kuongoza katika dakika ya 28 ndani ya kipindi cha kwanza.

Bao la pili la Kimbunga liliweza kuwekwa kimyani na mchezi Khalfan Mgeni ndani ya dkika ya 58 ya kipindi cha pili mara baada ya pasi safi kutoka kwa Idrisa Simai, na kwa upande wa Jang’ombe boys bao la kufutia machozi lilifungwa na Abrahman       ... Read more »

Views: 208 | Added by: salminjsalmin | Date: 02.18.2016 | Comments (0)


Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz