Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
9:23 AM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 18 » BOYS WASHINDWA MBELE YA KIMBUNGA.
6:33 AM
BOYS WASHINDWA MBELE YA KIMBUNGA.

 

Timu ya Jang’ombe boys imeshindwa kutamba baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Kimbunga katika mchezo uliosukumwa jana jioni majira ya saa kumi ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar ambao ni muendelezo mwa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja.

Katika mchezo huo uliojaa mashabiki kiwanjani timu hizo zilionesha kandanda safi kwa kufanya mashambulizi kila mara, na ndipo Waziri Ramadhan alipoweza kuipatia kimbunga bao la kuongoza katika dakika ya 28 ndani ya kipindi cha kwanza.

Bao la pili la Kimbunga liliweza kuwekwa kimyani na mchezi Khalfan Mgeni ndani ya dkika ya 58 ya kipindi cha pili mara baada ya pasi safi kutoka kwa Idrisa Simai, na kwa upande wa Jang’ombe boys bao la kufutia machozi lilifungwa na Abrahman         Othman mnamo dakika ya 81 ya mchezo huo.

 

Katika mzunguko wa mwanzo timu hizo ziliweza kukutana na Jang’ombe boys walikubali kufungwa na Kimbunga mabao kama hayo 2-1, na wameweza kuendeleza tena uteja wao kwa Kimbunga baada ya jana kufungwa tena.

Kwa matokeo hayo Jang’ombe wapo nafasi ya tisa 9 na alama kumi na sita (16), huku Kimbunga wakipanda hadi nafasi ya nane (8) na alama zao ni kumi na saba (17).

 

Views: 208 | Added by: salminjsalmin | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar

Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz