Mabaharia wa KMKM,wamewazabua Kipanga mabao matano kwa moja 5-1 katika mchezo wa muendelezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja uliosukumwa jana jioni ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar.

Katika mchezo huo timu ya Kipanga iliovalia jezi rangi nyeupe, ilionekana kucheza chini ya kiwango, na kuweza kushambuliwa na KMKM mara kwa mara katika lango lao, na ndipo mchezaji Mudrik Muhib alipoanza kupachika bao la kwanza ndani ya dakika ya 19 .
...
Read more »