Ligi kuu ya soka ya La Liga nchini Uhispania iliwakutanisha Real Madrid na Atletico Bilbao kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.

Kocha wa Real Madrid Zinadine Zidane aliendeleza rekodi yake ya kutoshindwa nyumbani na kuhakikisha timu yake inapata ushindi na pointi 3.
Real Madrid iliweza kushinda mechi hiyo 4-2 baada ya kufungiwa magoli yake na Ronaldo (dakika ya 3 na 87), Rodriguez (dakika ya 37) na Kroos (dakika ya 45).
Wageni Atletico Bilbao nao walifunguwa magoli yao na Eraso (dakika ya 11) na Elustondo (dakika ya 90).
Wakati huo huo, Real Madrid walilazimika kumaliza mechi hiyo wakiwa wachezaji 10 baada ya Varane kuonyeshwa kadi nyekundu iliyojumuisha kadi mbili za njano katika dakika ya 83.
|