
Kikosi cha Yanga kilitua jana nchini Mauritius kwa ajili ya mechi yao ya kimataifa ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya timu ya Cercle de Joachim ya nchini humo mchezo wa raundi ya awali.
Yanga watacheza leo mchezo huo kisha kukwea pipa na kutimkia kisiwani Zanzibar kwa ajili ya kambi ya kujifua kuwakabili watani zao wa jadi Simba SC mchezo utakaopigwa February 20 kwenye uwanja wa taifa.
Vijana wa Jangwani wameonekana kwenye mitaa ya Mauritius wakiwa na furaha huku wakipiga picha kwa ajili ya kumbukumbu zao za baadae.
chanzo:shaffih dauda.
|