Wakati huo huo kocha wake huyo wa zamani pia anaamini Mudathir huwenda akaja kuchezea tena timu kubwa za Tanzania ikiwemo Yanga alipoachwa na mwisho wake hadi kudakia Taifa Stars.
“ Timu kubwa za Tanzania zitamuhitaji tu baadae Mudathir, hasa awo Yanga walomuacha kwasababu ni hodari na hata siku moja atakuwa Tanzania one ndani ya timu ya Taifa”. Alisema Salum ambae pia aliwahi kuwa mlinda mlango wa Malindi, KMKM na Zanzibar Heroes.

Mudathir tayari ameshanza kuidakia timu yake mpya ya Mgambo Shooting michezo kadhaa ambapo hata katika mchezo uliopigwa February 3 mwaka huu alikaa yeye langoni walipopigwa 5-1 na Simba kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara ambapo akionekanwa matumaini yakufanya vizuri yanafufuka kufuatia kuwa kama mzigo mzunguko wa kwanza alipokuwa akikipiga Yanga tofauti alipochukuliwa kwa shangwe akiwa kipa namba moja katika klabu ya KMKM.