Amesema kwamba ni vyema walimu wanapoandaa michezo kwa ajili ya elimu bila ya malipo wanatakiwa kuzingatia sana maadili ili kusiwepo na upotoshwaji wa tamasha hilo .
Aidha amewataka walimu kutambua dhamana zao jambo ambalo litasaidia kudumisha nidhamu kwa wanafunzi .
Naye Afisa Michezo na Utamaduni Wilaya hiyo amewataka walimu hao kuanza maadalizi mapema kwa kuangazlia vipengele muhumi ambavyo vinaweza kusaidia skuli zao kupata ushindi .
Kikao hicho ni maandalizi ya Tamasha la Elimu bila ya malipo ambalo kwa Pemba linatarajia kuzinduliwa tarehe 13 mwezi huu katika wilaya ya chake chake.