Wiki ya 26 ya ligi kuu ya soka ya EPL nchini Uingereza ilitamatishwa kwa mechi kali ya kusisimua kati ya Manchester City na Tottenham Hotspur iliyochezwa uwanjani Etihad.
Manchester City iliyoyumba wiki iliyopita, iliendelea kusambaratika nyumbani kwa kushindwa kupata pointi.
Tottenham Hotspur yazidi kukomaa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania taji la EPL

Wageni Tottenham Hotspur walionyesha mchezo mzuri na kufanikiwa kuondoka na pointi 3 baada ya kuilaza Manchester City 2-1.
Tottenham Hotspur ilitangulia kufunga goli la kwanza kwa mkwaju wa penalty kupitia Harry Kane katika dakika ya 54 kabla ya Iheanacho kusawazisha katika dakika ya 74.
Eriksen aliiletea ushindi Tottenham Hotspur baada ya kupachika goli la pili katika dakika ya 83.
|