United walichapwa mabao 2-1 na timu ndogo ya Midtjylland.
Klabu hiyo ya Old Trafford pia ilipata pigo baada ya kipa wake namba moja David de Gea kuumia kifundo cha mguu wakati akipasha mwili moto na nafasi yake kuchukuliwa na Kipa wa Argentina Sergio Romero.
Man Utd walitangulia kufunga kupitia Memphis Depay lakini Midtylland wakasawazisha kupitia Pione Sisto na Paul Onuachu alifunga bao la ushindi.
Manchester United walishindwa na Sunderland 2-1 Jumamosi Ligi ya Premia na wamepungukiwa na alama sita kufikia nambari nne, nafasi ya kufuzu Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Meneja wao Louis van Gaal majuzi alisema kushinda Europa League ndio njia rahisi kwao kufuzu kwa ligi hiyo ya mabingwa Ulaya msimu ujao.
Kwenye mechi nyingine zilizochezwa Alhamisi usiku, Borrusia Dotmund wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani, walipata ushindi wa 2-0 dhidi ya FC Porto
Matokeo mengine ni:
◾Tottenham 1-1 Fiorentina
◾Valencia 6-0 Rapid Vienna.
◾Liverpool 0-0 Augsburg.
◾Anderlecht 1 –0 Olympiakos
◾Sevilla 3- 0 Molde
◾St Etienne 3-2 Basel
◾Villarreal 1- 0 Napoli
◾FC Sion 1-2 Sporting Braga
◾Galatasaray 1-1 Lazio
◾Marseille 0-1 Ath Bilbao