Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
10:34 AM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 2
Guests: 2
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 16 » KVZ YAANZA VYEMA MZUNGUKO WAKE WA PILI
6:54 AM
KVZ YAANZA VYEMA MZUNGUKO WAKE WA PILI

Timu ya KVZ,  imeanza vyema katika mzunguko wake wa pili baada ya kuicharaza Mtende mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja uliosukumwa jana jioni ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar.

Katika mchezo huo mchezaji Abdillah Seif Bausi alianza kuipatia KVZ bao la kwanza ndani ya dakika ya 26 baada ya kuupiga mpira wa adhabu nje ya 18 iliyotokana na mchezaji wa Mtende Ali Mwinyi kumfanyia madhambi mchezaji wa KVZ Abbas Abdallah, na bao la pili liliwekwa kimyani na mchezaji Emill Willium mnamo dakika ya 58 ya mchezo huo.

KVZ waliwahi kukutana na Mtende katika mzunguko wa mwano na KVZ waliibuka na ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Mtende.

Kwa matokeo hayo timu ya KVZ imepanda hadi nafasi ya tatu 3 wakiwa na alama 23, huku Mtende wakiendelea kuburura mkia wakiwa na alama sita.

Views: 172 | Added by: salminjsalmin | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar

Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz