Home
Sign Up
Log In
Monday
06.23.2025
1:36 PM
Welcome Guest | RSS

            SALMA SPORTS MEDIA


    PATA HABARI MOTOMOTO ZA MICHEZO NDANI NA NJE YA

NCHI. 

                                                                                                                 TANGAZA NASI



WASILIANA NASI KUPITIA +255 779 518 500 / +255 772 997 018 / +255 678 043 812; email: salmahassan040@gmail.com / salminjsalmin@gmail.com



Site menu

Our poll
Rate my site
Total of answers: 3

Statistics

Total online: 1
Guests: 1
Users: 0

  
Home » 2016 » February » 19 » JKU NA MAFUNZO ZASHINDWA KUTAMBIANA.
7:17 AM
JKU NA MAFUNZO ZASHINDWA KUTAMBIANA.

 

Timu ya Jeshi la kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) na Mafunzo jana zimeshindwa kutambiana katika mchezo wa muendelezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja, baada ya kutoka sare ya bila kufungana katika mtanangde ambao uliosukumwa ndani ya dimba la Amani mjini Zanzibar.

Katika mchezo huo uliokuwa na hamasa za mashabiki kiwanjani hapo timu zote zilionekana kucheza mpira wa hali ya juu kwa kufanya mashambulizi, lakini timu zote zilionekana k...uwa imara kwenye safu yao ya ulizi kwa kipindi chote kwa kutokuruhusu bao kuweza kupenya kwenye lango lao.

Ndani ya dakika ya 44 ya mchezo huo, mchezaji wa Mafunzo Juma Othman Mmanga aliweza kumfanyia faulu mchezaji wa JKU Mbarouk Chande wakati alipokuwa kwenye harakati za kutaka kufuga bao ndani ya eneo la hatari, na ndipo mwamuzi wa pambano hilo Issa Haji alipoamua upigwe mkwaju wa penalt kuelekea kwenye lango la Mafunzo, lakini Mbarouk Chande alishindwa kuuzamisha wavuni mpira huo baada ya mlinda mlango wa Mafunzo Abdul-swamad Suleiman kuutoa mpira huo.

Katika kipindi cha pili timu zote ziliweza kufanya mabadiliko kwa kuwatoa wachezaji wake lakini mabadiliko hayo hayakuweza kuzaa matunda kwa timu zote kwani hadi mtanange huo ulipomalizika timu hizo zimetoka sare ya bila kufungana.

Timu hizo katika mzunguko wa mwanzo ziliweza kukutana na JKU waliweza kuwafunga Mafunzo mabao 2-1 katika ligi hiyo.

Mafunzo wakiwa ndio bingwa mtetezi wa ligi hiyo bado akionekana kususa msimu huu ambao wamepishana kwa alama kumi na tatu (13) na kinara wa ligi hiyo.

Kocha msaidizi Abdalla Bakar Eddo, amewataka mashabiki wake kuwa wasikate tama kwani taji hilo watalitetea bila ya wasiwasi wowote ule.

Kwa matokeo hayo timu ya JKU imebakia kileleni wakiwa na alama (32), huku bingwa mtetezi timu ya Mafunzo wao wakiwa nafasi ya saba na alama kumi na tisa (19).

Views: 220 | Added by: salminjsalmin | Rating: 0.0/0
Total comments: 0
avatar

Visitors
idadi ya watembeleaji
Idadi ya watembeleaji

WATEMBELEAJI

Entries archive

Salma Sport Media © 2025
uCoz