Mara baada ya majigambo ya msemaji wa Black sailors ya kusema kuwa watashinda katika mechi yao kati ya Polisi hatimae wakubali kutoka sare katika mchezo huo.
Timu ya Black sailors na Polisi leo zimeshindwa kutambiana katika mchezo wa muendelezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja,baada ya kutoka sare ya bila kufungana.Katika mchezo huo timu zote zilionekana kutafuta alama tatu muhimu katka ligi hiyo.

Black sailors iliyovalia jezi rangi nyeusi na Polisi imevalia jezi rangi nyeupe.
Kocha wa timu ya kikosi cha Polisi Ali Suleiman Mtuli amesema kuwa, hawakutakiwa kutoka sare katika mchezo huo ila walitakiwa washinde lakini ameongeza kwa kusema kuwa bado kuna matatizo katika kikosi chake hivyo wanatakiwa wayatatue ili waweze kujinasua katika kushuka daraja.
Aidha kwa upande wake kocha wa black sailors amesema Juma Awadh,amesema waliweza kupata nafasi za kufunga lakini nafasi hizo timu yake imeshindwa kuzitumia vizuri, lakini ndo mpira kwani bahati haikuwa ya kwao na wao wameyakubali matokeo hayo.
Timu ya Polisi ambayo bado inaonekana kusuasua katika ligi kuu ya Zanzibar imeshacheza michezo kumi na nne (14) wakiwa nafasi ya kumi na tatu 13 na alama na 8, huku Black sailor wao wakiwa na alama (22) wakishika nafasi ya nne (4).
Huu ni mzunguko wa pili katika ligi kuu ambao ni wa lala salama ambapo mzunguko wa mwanzo timu hizi zilipokutana Black sailors walifanikiwa kuwafunga maafande hao wa Polisi.
|