Kwa upande wa JKU wao wakiwa ndio kinara wa ligi hiyo wataingia uwanjani wakiwa na alama (32), wamepoteza mchezo mmoja katika michezo kumi na tatu (13) waliyocheza huku wakitoka sare michezo miwili, wakati Black sailors wao wataingia uwanjani wakiwa wamecheza michezo kumi na nne (14), wameshinda michezo sita (6), sare michezo minne (4) na wamepoteza minne (4),wanakamata nafasi ya tano (5) na alama zao ni (23).